Pangani FM
Pangani FM
09/03/2026, 13:58

Na Cosmas Clement
Mbunge wa jimbo la Pangani na waziri wa maji Mhe. Juma Hamidu Aweso hii leo amekabidhi mashine moja ya kudurufu nakala (photocopy machine) yenye thamani ya shilingi milioni nane kwa shule ya sekondari Muhembo iliyopo kijiji cha Pangani Mashariki wilayani Pangani.
Akikabidhi mashine hiyo kwa niaba ya mbunge huyo, Katibu wa mbunge wa jimbo la Pangani Mwl. Salmini Mmari kutolewa kwa mashine hiyo ni muendelezo wa jitihada za kuboresha kiwango cha ufaulu katika wilaya ya Pangani.
Mkuu wa shule ya sekondari Muhembo Mwl. Ernesta Mwakamela amesema kupatikana kwa mashine hiyo itasaidia kupunguza changamoto za upatikanaji wa huduma za uchapishaji wa mitihani.

Bwana Peter Mabuga mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari ya Muhembo amemshukuru Mbunge huyo kwa kutoa mashine hiyo akiwaasa wanafunzi na walimu kuitunza mashine hiyo iweze kudumu kwa muda mrefu.
Ofisi ya mbunge wa jimbo la Pangani imekuwa ikitoa misaada mbalimbali inayolenga kutatua changamoto za kielimu ili kuinua sekta ya elimu wilayani humo.