Pangani FM

Je unajua yalipo mafanikio yako?

16 February 2026, 11:46 pm

Picha ya baadhi ya wanandoa wakiwa katika mafunzo saidizi yaliyotolewa na shirika la UZIKWASA. Picha na Eric Malya.

Hapo mwanzo tulikuwa tumepanga lakini baada ya migogoro yetu kuisha tumejenga nyumba na tumenunua shamba.

Na Cosmas Clement

Uwezo wa wanandoa kushughulikia migogoro baina yao imetajwa kuwa chachu ya kuwawezesha kupiga hatua za maendeleo katika familia zao.

Hayo yamesemwa na wenza walioshiriki katika mafunzo saidizi yanayotolewa na shirika la UZIKWASA kwa wenza zaidi ya 28 kutoka maeneo mbalimbali wilayani Pangani.

Wakizungumza katika mafunzo hayo wenza hao wamesema kutokana na mabadiliko waliopata baada ya mafunzo ya wenza yamewawezesha kutatua migogoro iliyokuwa ikiwakabili hivyo kuwawezesha kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo ya familia.

sauti wenza

Hata hivyo, wamesema mafunzo saidizi waliopatiwa hii leo yamesaidia kuwajengea uwezo wa  kuondoa baadhi ya changamoto walizonazo ikiwemo kutokuaminiana.

Sauti ya wenza

Kwa upande wake Bwana Joseph Peniel mwezeshaji kutoka UZIKWASA amesema maelewano mazuri kwa wanandoa huwezesha  kupanga kwa pamoja hivyo kupiga hatua katika maendeleo ya familia.

Sauti ya bwana Joseph Peniel mwezesha kutoka UZIKWASA