Pangani FM

Pangani kuanza mradi, nishati safi ya kupikia

10 June 2024, 9:28 pm

Jiko la gesi, moja ya nishati safi ya kupikia

Mradi wa nishati safi ya kupikia utawawezesha wananchi wa Pangani kunufaika na biashara ya hewa ya ukaa.

Na Majabu Madiwa

Shirika la kuhifadhi misitu ya asili nchini Tanzania (TFCG) limeanza kutambulisha mradi wa nishati safi katika halmashauri ya Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga.

Hayo yamesemwa na afisa mazingira Wilaya ya Pangani BW DAUDI MLAHAGWA ambapo amevitaja vijiji vitakavyonufaika ni Mseko Mtango na Kwakibuyu.

Sauti ya afisa mazingira wilaya ya Pangani Bwana Daudi Mlahagwa

Aidha BW MLAHAGWA amesema ujio wa wadau mbalimbali wa mazingira Wilayani Pangani utaendelea kuchagiza umuhimu wa utunzaji wa mazingira.

Sauti ya afisa mazingira wilaya ya Pangani Bwana Daudi Mlahagwa

Hatua hii ni jitihada za halmashauri katika kutafuta wadau wa nishati safi ambapo tayari mradi huo umekwisha tambulishwa katika ngazi ya Wilaya na hatua iyiyopo kwa sasa ni utambulisho wa mradi katika ngazi ya vijiji huku wananchi wakitarajiwa kunufaika  kupitia bishara ya hewa ukaa.