Orkonerei FM
Orkonerei FM
28 August 2026, 3:32 pm

picha kwa msaada wa mtandao
Afisa Kilimo kutoka Wilaya ya Simanjiro, Jenifar Mbuya, amewataka wakulima mkoani humo kufuata kanuni na misingi bora ya kilimo ili kujiwekea mazingira ya kupata mavuno mengi na yenye tija.
Na Dorcas Charles
Akizungumza na Mwandishi wetu Dorcas Charles amesema taratibu sahihi za uandaaji wa mashamba na upandaji, Afisa Kilimo huyo ameeleza kuwa ili mpeto au mavuno ya mkulima yawe yenye tija, mkulima anapaswa kuandaa shamba lake mapema kwa kutumia trekta na kufuata kanuni sahihi za upandaji badala ya kutumia njia zisizo rasmi.
Afisa Mbuya amebainisha kuwa wakulima wengi wamekuwa wakifanya makosa wakati wa upandaji kwa kufuatisha mbegu nyuma ya trekta badala ya kutumia jembe la mkono au kifaa maalum cha kupandia (planter).
Kulingana na maelezo yake, kufuata trekta wakati wa kupanda kunasababisha changamoto zifuatazo: