Orkonerei FM

Minara ya Simu inavyofungua Fursa za Biashara Vijijini

14 November 2025, 3:17 pm

Muonekano wa minara ya simu (Picha kwa msaada wa Mtandao)

Kipindi hiki cha Kurunzi Maalum kinachambua jinsi ongezeko la minara ya simu nchini Tanzania linavyobadilisha upatikanaji wa mawasiliano, hasa vijijini.

Kwa mujibu wa TCRA, Tanzania imefikia zaidi ya minara 10,000 ya mawasiliano, huku UCSAF ikiendelea kupanua huduma vijijini kupitia miradi inayofikia zaidi ya wananchi milioni 8.5.

Kupitia simulizi, mahojiano na uchambuzi wa kitaalamu, kipindi kinaonyesha jinsi miundombinu hii inavyowezesha vijana na wafanyabiashara kutumia mitandao ya kijamii kama chanzo cha kipato badala ya burudani pekee.

Makala ya kurunzi wiki hii kuhusu ujenzi wa minara na masoko ya kimtandao