Pangani FM

Waaswa kutowanyanyapaa wenye matatizo ya afya ya akili

27 March 2026, 13:50

Picha kutoka mtandaoni

Hapa kwetu tuna vituo 33 vya kutolea matibabu ya afya ya akili, ambavyo vinajumuisha vituo vyote vya kutolea huduma za afya kuanzia ngazi ya Zahanati hadi hospital

Na Mwandishi Wetu

Wananchi katika wilaya ya Tanga, mkoani Tanga wameaswa kuepuka kutumia majina yanayowanyanyapaa wenye changamoto ya matatizo ya afya ya akili kwani ni matatizo yanayoweza kumpata mtu yoyote.

Hayo yamesemwa na Mratibu wa afya ya akili Jiji la Tanga Dkt George Semsela, kufuatia uwepo wa baadhi ya watu kutumia maneno potofu dhidi ya watu wenye matatizo ya afya ya akili.

Sauti ya Mratibu wa afya ya akili Jiji la Tanga Dkt George Semsela

Amesema changamoto ya matatizo ya afya ya akili ni kubwa huku akielezea idadi ya watu waliohudhuria hospitali kwa ajili ya changamoto hiyo.

Sauti ya Mratibu wa afya ya akili Jiji la Tanga Dkt George Semsela

Amewasihi wanajamii kuondokana na mitazamo ya imani za kishirikina juu ya changamoto ya afya ya akili na  kuchukua hatua madhubuti kujiupusha na vihatarishi vinavyopelekea matatizo hayo.

Sauti ya Mratibu wa afya ya akili Jiji la Tanga Dkt George Semsela