Pangani FM

Pangani kuvuka lengo la serikali la upandaji miti

17/03/2026, 19:19

Miche ya miti ikiwa katika viriba: picha Tovuti ya TFS

Na Cosmas Clement

Halmashauri ya wilaya ya Pangani imesema inatarajia kuvuka lengo la serikali la kupanda miti mil 1.5  mwaka huu ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha wiki ya upandaji miti duniani ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Akizungumza na Pangani FM kwa njia ya simu Mkuu wa idara ya maliasili na mazingira bwana Twahiru mkongo amesema kuelekea wiki hiyo wamepanga kufanya zoezi la upandaji wa katika shule ya msingi Bushiri kwa kupanda miti zaidi ya mia tano.

Mkuu wa idara maliasili na mazingira Twahiru Mkongo

Bwana Mkongo amesema mpaka sasa wilaya kwa kushirikiana na wadau wamefanikiwa kupanda miti zaidi ya milioni moja aina ya mikoko.

Mkuu wa idara maliasili na mazingira Twahiru Mkongo

Hatua hiyo inakuja katika kuekeleza kilele cha wiki ya upandaji miti duniani ambapo tayari wilaya ya Pangani imesha sambaza miche ya miti mbalimbali katika vijiji vilivyopo wilayani humo.