Pangani FM
Pangani FM
17/03/2026, 12:34

Na Saa Zumo
Rushwa inatajwa kuchangia kukwamisha kesi za ukatili wa kijinsia kata ya Kabuku Wilayani Handeni mkoani TANGA.
Hayo yamezungumzwa na baadhi ya wajumbe wa kamati zya MTAKUWWA kata ya Kabuku wilayani Handeni ambapo wamesema wanakumbana na ugumu wa kutokomeza changamoto ya matukio ya ukatili kutokana na wahalifu wa vitendo vya ukatili kutajwa kutoa Rushwa ili kesi zisiendelee.
Ili kufanikisha mapambano dhidi ya kushughulikia kesi za ukatili katika eneo la Kabuku wajumbe wameshauriwa kutunza siri ili kufanikisha utatuaji wa matukio hayo.
Mmoja kati ya mjumbe ambaye ni mwalimu katika shule ya sekondary katika kata hiyo amesisitiza jamii kutenga muda wa kuwasikiliza watoto ili kutambua changamoto zinazowakabili.