Pangani FM
Pangani FM
17 February 2026, 6:26 pm

“Mimi baada ya mafunzo haya nitakaa na vijana wangu pale ofisi ili niwaeleze njia sahihi za matumizi ya vyeo na nafasi zetu“
Na Cosmas Clement
Matumizi yasiyo sahihi ya vyeo na nafasi kwa viongozi vimetajwa kuwa miongoni mwa mikwamo ya kutoa huduma bora kwa wananchi wanawaongoza.
Hayo yamesemwa na washiriki wa mafunzo ya uongozi yanayotolewa na shirika la UZIKWASA kwa wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri ya Handeni kwa lengo la kuwawezesha kutumia mbinu wezeshi katika kutatua changamoto za kijamii na kuimarisha mahusiano ya na jamii.
Katika mafunzo hayo washiriki waliwezeshwa katika kufahamu matumizi sahihi ya vyeo na nafasi pamoja na tathimini binafsi hivyo kuwawezesha kugundua maeneo ya kufanyia kazi.

Kwa upande wake meneja wa ufuatiliaji na tathimini na mwezeshaji wa shirika la UZIKWASA bwana Joseph Peniel amesema kupitia mafunzo hayo wanatarajia kuona mabadiliko ya kiutendaji kwa washiriki hao wa mafunzo.
Mafunzo ya uongozi wa Mguso kwa wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri ya wilaya ya Handeni yameanza leo na yanatarajiwa kuhitimishwa kesho.