Pangani FM

Ukusanyaji mapato mazao ya misitu ya vijiji yawaibua madiwani Pangani

2 August 2024, 9:58 pm

Katikati aliyesimama ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani Mhe, Akida Bahorera akiwa katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Pangani.

Wakala wa Huduma za Misitu umeundwa kwa madhumuni ya kuhakikisha; Uwepo wa usimamizi madhubuti na wenye ufanisi na tija wa rasilimali za misitu na nyuki, kuongeza ubora na thamani ya kifedha katika kutoa huduma kwa umma; na kuendelea kukuza na kuboresha uwezo wa kutoa huduma kwa umma.

Na Cosmas Clement

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Pangani Mhesimiwa Akida Bahorera anatarajia kukutana na baadhi watumishi na madiwani kutafuta suluhu la ukusanyaji wa ushuru wa mazao ya misitu ya vijiji.

Hatua hiyo imetokana na hoja iliyoibuliwa na Diwani wa kata ya mikinguni Mheshimiwa Joel Mrutu, katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika julai 31 mwaka huu katika ukumbi wa halmashauri ya zamani ya wilaya ya Pangani.

Sauti ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Pangani Mhe, Akida Bahorera

Katika hoja yake Mheshimiwa Joel alieleza kuwa kuna baadhi ya vijiji vinaendesha shughuli za uvunaji wa msitu wake wa asili lakini hawahusiki kukusanya ushuru wa mazao ya msitu huo.

Sauti ya Mhe Joel Mrutu diwani wa kata mikinguni

Kwa upande wake Meneja Muhifadhi TFS Bwana Eliapenda Wavii ameelezea jinsi TFS inavyowajibika katika ukusanyaji wa mapato ya mazao ya misitu.

Sauti ya Eliapenda Meneja muhifadhi TFS Pangani