Pangani FM

Zingatia haya kuimarisha afya yako

25 July 2024, 3:28 pm

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Pangani Mashariki Bi Lilian Mwenye mtandio wa rangi ya krimu akifuatilia upishi wa uji wa lishe katika maadhimisho ya siku ya afya na lishe katika kijiji hicho.

Siku ya Afya na Lishe inapaswa kufanyika kwa kila kijiji mara nne kwa mwaka kwa vipindi vya miezi mitatu ili kutoa elimu kwa jamii juu ya milo sahihi.

Na Cosmas Clement

Wananchi katika kijiji cha Pangani Mashariki wametakiwa kuzingatia lishe bora ili kupunguza changamoto za kutozingatia lishe ikiwemo upungufu wa damu kwa wakinamama wajawazito.

Hayo yameelezwa na Afisa lishe wilaya ya Pangani Bwana Daudi Mwakabanje ambapo ametanabaisha uwepo wa  tatizo la udumavu kwa watoto na upungufu wa damu kwa wanawake kipindi cha ujauzito.

Daudi mwakabanje afisa lishe wilaya ya Pangani

Kwa upande wake Mtendaji kata ya Pangani Mashariki Bwana Mponji Kaziyabwana amesema Kata hiyo imesaini Mkataba na ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Pangani juu ya utekelezaji wa afua za lishe.

Sauti ya Kaziyabwana Mponji

Nao wakazi wa kijiji hicho waliohudhuria maadhimisho hayo wameelezea kupata elimu ya lishe bora itakayowawezesha kufuata milo sahihi katika familia zao.

Sauti ya wakazi wa P/MASHARIKI

Maadhimisho ya siku ya afya na lishe ngazi ya kijiji hufanyika kila baada ya miezi mitatu kwa mwaka. Ambapo kijiji cha Pangani Mashariki hapo jana kimeadhimisha siku ya afya na lishe.