Pangani FM
Pangani FM
16 July 2025, 11:25 am

“Ni vyema jamii ikaacha kuwatenga vijana waliojiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya na kuwa karibu nao ili kuwawezesha kuacha kutumia dawa hizo na kubadili maisha yao.”
Na Abdilhalim Shukran
Jamii imeaswa kutowatenga vijana ambao wamejiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya badala yake imeshauriwa kuwapa elimu ya kujitambua.
Wito huo umetolewa na baadhi ya Vijana ambao waliopatiwa mafunzo ya kupinga ukatili na shirika la UZIKWASA wakati wa wakiwa kwenye kipindi cha Kona Ya Kijanja kinachorusha na kituo hiki.
Miongoni mwa vijana hao ni bwana Hassani Omary na bwana Burkhan Bakari ambapo wamesema ni vyema jamii ikaacha kuwatenga vijana waliojiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya na kuwa karibu nao ili kuwawezesha kuacha kutumia dawa hizo na kubadili maisha yao.
Aidha vijana hao wamebainisha sababubu zinazopelekea vijana wengi kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo makundi rika.
Kwaupande mwengine vijana hao wameshauri boda boda waliopatiwa mafunzo na shirika la UZIKWASA juu ya kupinga ukatili katika jamii zao kuendelea kuyafanyia kazi na kuendelea kuyaambukiza kwa wenzao.