Pangani FM

Fahamu faida watoto wenye mahitaji maalumu kupata elimu

26 June 2025, 10:38 am

Mkufunzi wa mafunzo ya ubainishaji watoto wenye mahitaji maalumu kutoka mradi wa shule bora akiwawezesha waratibu elimu kata wilaya ya Pangani

“lengo la mafunzo hayo ni kuwaibua watoto wenye mahitaji maalumu ili kutambulika na kujumuishwa katika elimu sawa na watoto wengine.”

Na Cosmas Clement

Halmashauri ya wilaya ya Pangani imeanza utekelezaji wa mpango wa elimu jumuishi chini ya mradi wa Shule Bora kwa kuwapa mafunzo waratibu elimu kata, yaliyolenga kuwawezesha kubainisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

Akizungumza na Pangani FM baada ya mafunzo hayo, mratibu wa mradi wa Shule Bora wilayani Pangani Mwl. Joseph Kyara amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaibua watoto wenye mahitaji maalumu ili kutambulika na kujumuishwa katika elimu sawa na watoto wengine.

Sauti ya mratibu wa mradi wa shule bora Pangani Joseph Kyara

Washiriki wa mafunzo hayo ambao ni waratibu elimu 14 za wilaya ya Pangani wamesema mafunzo hayo yamewapa ufahamu wa kusimamia elimu jumuishi katika maeneo yao ya kazi.

Sauti ya waratibu elimu kata
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalumu wilayani Pangani.

Kwa upande wake Mwl. Mathias Pori ambaye ni mratibu wa elimu maalumu wilayani Pangani amesema mafunzo yatasaidia kuwaibua watoto wengi wenye wenye mahitaji maalumu.

Sauti ya Mathias Pori mratibu elimu maalumu wilaya ya Pangani

Mafunzo hayo ya siku mbili yalianzia jumatatu na kuhitimishwa jana yanatarajiwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu inayojumuisha watoto wote kwa usawa.