Pangani FM

Wananchi waaswa kulinda miundombinu ya maji

18 June 2025, 1:55 pm

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ndugu Ismail Ally Ussi akiwa kati kati ya Mbunge wa jimbo la Pangani Mhe. Jumaa Hamidu Aweso na Mkuu wa wilaya ya Pangani Mhe. Gift Isaya Msuya

Naipongeza RUWASA kwa utekelezaji wa mradi huu na ushirikiano mnaouonesha, kuweka jiwe la msingi katika mradi huu ni kama nauonea mimi nilitaka kuuzindua kabisa kwa sababu ni mradi uliofuata hatua za utekelezaji.

Na Cosmas Clement

Wakazi wa vijiji vya mikocheni na Mkwaja vilivyopo wilaya ya Pangani wameaswa kuitunza miundombinu ya mradi wa maji wa Mikocheni ambao umewekewa jiwe la msingi na kwasasa umefikia asilimia 80 ya ujenzi.

Hayo yamezungumzwa na kiogozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa ndg Ismail Ali Usi wakati Mwenge ulipofika katika mradi huo na kuweka jiwe la msingi.

Sauti ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa ndg Ismail Ali Usi

Aidha ameipongeza RUWASA kwa utekelezaji wa mradi huo uliofuata matakwa na mahitaji ya wananchi katika eneo hivyo utasaidia kuondoa changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi.

Sauti ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa ndg Ismail Ali Usi