Pangani FM

RC Dkt Batilda azindua mnada wa ufuta Pangani

8 June 2025, 7:08 pm

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani

‘Sisi tuna uzoefu wa minada ya korosho hapa Tanga lakini baadae korosho zikawa zinatoroshwa kwenda nje ya mkoa wetu, ni kwa sababu tulifanya mnada mara moja haukuendelea.’

Na Cosmas Clement

Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani leo amezindua mnada wa ufuta katika kijiji cha Stahabu wilayani Pangani ambapo tani zipatazo tano 122.6  za wakulima zinatarajiwa kuuzwa siku ya jumatatu ya tarehe 9/6/2025.

Akizungumza katika uzinduzi wa mnada Dkt Batilda amewaasa wakulima kukusanya mazao yao katika mifumo rasmi ya ushirika ili kupata manufaa kiuchumi akiahidi kuhakikisha minada hiyo inakuwa endelevu.

Sauti ya Dkt Batilda Buriani mkuu wa mkoa wa Tanga

Mrajisi wa vyama vya Ushirika mkoa wa Tanga Bwana John Henjewele amesema kuzinduliwa kwa mnada huo kutawezesha kutangaza fursa ya uwepo mazao ya ufuta na kuimarisha minada ya mara kwa mara.

Sauti ya John Hejewele mrajisi wa ushirika Mkoa wa Tanga

Naye mkuu wa wilaya ya Pangani Mhe Gift Msuya amesema kuwa uwepo wa mfumo wa uuzaji wa mazao mchanganyiko kupitia mnada utasaidia kuondoa matapeli.

Sauti ya Mkuu wa wa wilaya ya Pangani Gift Msuya

Kwa upande wake Bwana Gread Saidi afisa kilimo kutoka mamlaka ya udhibiti wa Nafaka na mazao mchanganyiko  COPRA amezishauri Halmashauri kudhibiti mipaka ili kuia utoroshaji wa mazao nje ya mkoa.

Sauti ya Gread Saidi Afisa Kilimo COPRA

Uzinduzi wa mnada wa ufuta umefanyika katika ghala la Stahabu kupitia AMCOS ya MITUMWE.