Pangani FM

Doria zaimarisha uhai wa misitu Muheza

31 May 2024, 11:54 pm

Msitu uliyoimarika kwa kutunzwa na kusongwa na aina mbalimbali za miti: Picha kutoka Mtandaoni.

Watu wameacha kuharibu misitu kutokana na sheria tulizoweka pamoja na doria, kwa sasa hata kama ni baba au ndugu yako akiharibu msitu utampeleka mbele ya sheria.

Na Hamisi Makungu

Doria za mara kwa mara katika hifadhi ya misitu wilayani Muheza mkoani Tanga zachangia kupunguza uharibifu wa misitu na kupeleka kushamiri kwa hali ya ukijani katika misitu hiyo.

Wakizungumza na Pangani FM Redio baadhi ya wananchi wa Kijiji cha kwezitu wameelezea manufaa wanayoyapata kutokana na kufanyika kwa doria hizo huku pia wakielezea nafasi yao katika kulinda misitu hiyo.

Wananchi wa Kwezitu wakipongeza doria kulinda msitu

Bwana Athoni Mshihiri ni katibu wa kamati ya mazingira ambayo inajihusisha na doria hizo anaeleza namna dozia zinavyofanyika.

Katibu wa kamati ya mazingira bwana Mshihiri

Kwa upande wake mwenyekiti wa Kijiji hicho Lukas Shemainde amesema pamoja na doria hizo kusaidia kuimarisha misitu pia wanendelea kutoa elimu kwa wananchi na kuzisimamia sheria

Sauti ya Mwenyekiti wa doria bwana Lukas