Pangani FM

Wenza msiwekeane vikwazo kufanya kazi

31 May 2024, 11:37 pm

Baadhi ya wajumbe wa MTAKUWWA wa kijiji cha Mtango wakiwa katika mafunzo yanayotolewa na shirika la Uzima Kwa Sanaa.

Migogoro mingi imekuwa ikiibuka kutokana na changamoto ya wenza wa kike wanapopangiwa zamu za kulinda usiku katika kampuni ya mkonge.

Na Saa Zumo

Jamii ya Kijiji cha Mtango Wilayani Pangani mkoani Tanga imetakiwa kuona umuhimu wa wenza wao kufanya kazi kulingana na taaluma walizosomea ili kuepusha migogoro baina yao.

Hayo yamejiri wakati wa mafunzo ya tathimini yaliyotolewa na shirika la Uzima Kwa Sanaa (UZIKWASA) wiki hii kwa wajumbe wa kamati ya Mtakuwa kijijini hapo ambapo moja ya changamoto iliyoibuka ni migogoro baina ya wenza inayochangiwa na uwepo wa wanawake kufanya kazi ya ulinzi nyakati za usiku katika kampuni zilizopo kwenye eneo hilo.

Mmoja wa wajumbe wakichangia

Akichangia hoja hiyo mmoja wa washiriki amesema kuwa jamii bado haijatambua umuhimu wa wanawake kufanya kazi katika mazingira yeyote ikiwemo nyakati za usiku.

Maoni ya Wajumbe

Kwa upande wake mwezeshaji kutoka shirika la UZIKWASA ndugu Eduward Saguti akawashauri wajumbe hao kuona umuhimu wa wenza kufanya kazi ili kujipatia kipato.

Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya mtakuwa Kijiji cha Mtango wamejipanga kuweka mikakati ya kutoa elimu kwa wakina baba wote ambao wenza wao wanafanya kazi nyakati za usiku ili kutatua changamoto hiyo