Sibuka FM

Watoto watatu wafariki kwa kukosa hewa Busega

25 August 2025, 1:01 pm

Muonekano wa jiko la mkaa kwenye picha likiwa na moto Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Walezi/Wazazi tunalo jukumu kubwa la kuwalinda watoto wetu wakati wote bila kujali mazingira waliyopo ili kuwakinga na vitu vinyoweza kuzuilika maana watoto ni tunu ya taifa lijalo”. 

Na,Anitha Balingilaki 

Watoto  watatu wa  kutoka kwenye  familia tatu wawili wakiwa wa kitongoji kimoja  wamefariki dunia kwa kukosa hewa baada ya kujifungia kwenye tent ambalo ndani yake waliweka jiko la mkaa na tukio hilo limetokea kata ya Mkula wilayani Busega mkoani Simiyu.

Watoto hao walikuwa kwenye makambi ya waadventista na waliwasha jiko hili kupika uji na badae mvua ilianza kunyesha wakajifungia ndani ya tenti ambalo ndani yake kulikuwa na jiko la mkaa wakiwa na lengo la kuepuka baridi.

Wakizungumza na Sibuka fm, Esta Bugoye bibi wa marehemu Loveness,Yusuph Lameck Mzazi wa marehemu Passion na Veronica Paul bibi yake marehemu Marry wameeleza namna walivyopokea taarifa hizo.

Sauti ya wazazi na walezi wakielezea namna walivyolipokea hilo tukio

Wakizungumzia tukio hilo Mahangi Luhanya mkazi wa Mkula na Lucas Mashauri wametoa ushauri kwa jamii kwa  kila tent liwe na msimamizi ambaye ni mtu mzima wanapokuwa kwenye makambi yoyote ili kuepusha changamoto zinazoweza kuepukika.

Sauti ya watoa ushauri 

Tukio hilo limethibitishwa na mkuu wa mkoa wa Simiyu Annamringi Macha na kuwataja watoto hao kwa majina yao,Loveness Emmanuel Kilonzo  alikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu (9) Passion Yusuph alikuwa mwanafunzi wa darasa la saba (14) na Mary Jackson (12).

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Simiyu, Annamringi Macha akizungumzia tukio hilo na namna ya kuweka ulinzi hasa kwa watoto wawapo makambini