Sengerema FM

Polisi Sengerema yawataka wananchi kutoa taarifa ya matukio

6 August 2026, 10:02 am

Inspt. Alex  Joseph Mtwangi na Inspt. Mayeji Busumabu wakitoa elimu ya kutoa taarifa na kulinda amani ya nchi. Picha na Elisha Magege

Jeshi la polisi wilaya ya Sengerema kutoa taarifa za matukio ya uvunjifu wa amani hasa matukio ya ukatili dhiidi ya watoto katika jamii

Na,Elisha Magege

Jeshi la polisi wilaya ya Sengerema limeendelea kutoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia huku likiwataka wananchi kutoa taarifa za uvunjifu wa Amani na uwepo wa matukio ya kihalifu katika jamii.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Buyagu Polisi kata wa kata hiyo Inspt. Alex  Joseph Mtwangi amesema jeshi la polisi limeamua kufika maeneo yote yenye mikusanyiko kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kutoa taarifa pindi matukio ya uvunjifu wa Amani yanapotokea katika jamii.

Sauti ya Polisi kata wa kata ya Buyagu Inspt. Alex  Joseph Mtwangi

Kwa upande wake Inspt. Mayeji Busumabu amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii na kuacha kujiingiza kwenye mambo yasiyofaa ili waweze kutimiza malengo yao.

Sauti ya Inspt. Mayeji Busumabu

Naye mkuu wa Shule ya Sekondari Buyagu Mwl. Aurelian Sandi amelishukuru Jeshi la polisi kwa kufika shuleni hapo na kutoa elimu hiyo huku akilisihi jeshi hilo kufika mala kwa mala kutoa elimu ya masuala ya ukatili na kutunza Amani ya nchi hasa kwa vijana.

Sauti ya mkuu wa Shule ya Sekondari Buyagu Mwl. Aurelian Sandi

Aidha jeshi la polisi wilayani Sengerema limewataka wananchi kuilinda Amani iliyopo na kufanya kazi ili kujiingizia kipato.