Sengerema FM

Wananchi watakiwa kuimalisha Ulinzi shirikishi

29 July 2026, 8:14 pm

ASP. Valentine Filimon Sarakikya akitoa elimu kwa wananchi juu ya ulinzi shirikishi.Picha na Elisha Magege

Kufuatia uwepo wa matukio ya uvunjifu wa amani katika jamii wananchi wametakiwa kushirikiana na jeshi la polisi katika wilaya ya Sengerema.

Na,Elisha Magege

Wananchi wametakiwa kushirikiana na jeshi la polisi kutoa taarifa za uharifu na waharifu ili kuinua shughuli za maendeleo katika jamii.

Akizungumza na wananchi kata ya Buzilasoga mratibu wa polisi Jamii wilaya ya Sengerema ASP. Valentine Filimon Sarakikya, wakati wa zoezi la kufanya usafi katika kituo cha afya Kanyerere amesema ili wananchi wapate maendeleo wanahitaji utulivu na amani, hivyo ni vyema jamii kuwafichua waharifu na kutoa taarifa za uharifu mapema.

Sauti ya mratibu wa polisi Jamii wilaya ya Sengerema ASP. Valentine Filimon Sarakikya

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Buzilasoga Bi.Edina Bandihai Amelipongeza jeshi la polisi kwa kufika na kutoa elimu ya ulinzi shirikishi, huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo.

Sauti ya Diwani wa kata ya Buzilasoga Bi.Edina Bandihai

Hata hivyo baadhi ya wananchi wa kata hiyo wamelishukuru jeshi la polisi wilaya ya Sengerema kwa kufika na kujumuika nao katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira.

Sauti za baadhi ya wananchi wa kata ya Buzilasoga

Jeshi la Polisi wilaya ya Sengerema linaendelea na falsafa yake ya kuwaweka pomoja, polisi na jamii katika mashirikiano ya kuleta maendeleo.

ASP. Valentine Filimon Sarakikya akifanya usafi na wananchi kata ya Buzilasoga.Picha na Elisha Magege