Sengerema FM
Sengerema FM
12 May 2026, 7:08 pm

Baada ya kuibuka kwa tabai za baadhi ya wataalamu wa tiba asili kuwatapeli wateja wao Mwenyekiti wa Chama cha Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Sengerema atoa onyo dhidi yao wanaojipatia pesa kwa njia ya udanganyifu.
Na,Emmanuel Twimanye
Waganga na wakunga wa tiba asili Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza wametakiwa kuacha tabia ya kutoa masharti magumu kwa wateja wanaofika katika maeneo yao kwa ajili ya kupata huduma za matibabu, kwa lengo la kuwatapeli fedha zao.
Onyo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Wilaya ya Sengerema, Juzaki Juzaki, kufuatia kuwepo kwa baadhi ya waganga wanaodaiwa kutumia njia hiyo ili kuwatapeli wananchi.
Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amewahakikishia wananchi kuwa waganga matapeli watachukulia hatua za kisheria ili kudhibiti suala hilo.
Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wameiomba serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria waganga matapeli,ili kukomesha tabia hiyo.