Sengerema FM
Sengerema FM
15 May 2026, 8:01 pm

Katika kukomesha tabia za baadhi ya watoto kujihusisha na vitendo vya wizi, wazazi na walezi Wilayani Sengerema wametakiwa kutoa malezi bora ili kuepuka kujihusisha na vitendo hivyo vinavyoweza kuhatarisha maisha yao.
Na, Emmanuel Twimanye
Watoto wawili wenye umri wa miaka 12 na 16 wamekamatwa katika mtaa wa Igogo Kata ya Nyampulukano Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza kwa tuhuma za wizi wa vitu mbalimbali .
Wakizungumzia tukio hilo wakiwa chini wa ulinzi wa polisi jamii watoto hao wamekiri kuiba vitu mbalimbali na kueleza kuwa hiyo ni mara yao ya pili.
Mwanamke aliyebiwa vitu hivyo Elizabeth Gidion amesema watoto hao waliruka ukuta kisha kuingia ndani na kuiba dish linalokadiliwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi laki tatu.
Wazazi wa watoto hao wamesikitishwa na watoto wao kujihusisha na vitendo vya wizi na kuiomba serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria ili liwe fundisho kwa watu weengine wenye tabia hiyo.
Kamanda wa polisi jamii kata ya Nyampulukano Lenatus Lugadija amethibitisha kukamatwa kwa watoto hao kwa tuhuma za wizi na kuwaonya vijana kuachana na vitendo vya wizi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Mtaa wa Igogo Goodluck Daud amewataka wazazi kuwa makini na malezi ya watoto wao watoto ili kuepuka kujihusisha na vitendo hivyo vinavyoweza kuhatarisha maisha yao.