Sengerema FM

Zima moto waonya wananchi kutoa taarifa za uongo

4 May 2026, 12:09 pm

Picha ya Konstebo Erick Karumuna akitoa elimu kwa wananchi, Picha na Emmanuel Twimanye

Jeshi la zima moto Sengerema latoa elimu kwa wanchi kuhusiana na matumizi sahihi ya namba za kutoa taarifa za dharula kwa jeshi hilo

Na:Emmanuel Twimanye

Wananchi Wilayani Sengerema mkoani Mwanza wameonywa kuacha kuchezea namba za dharura za Jeshi la Zimamoto na kutoa taarifa za uongo za matukio ya moto.

Onyo hilo limetolewa na Mkuu wa Jeshi la zima moto na uokoaji  wilayani Sengerema, Inspekta Juma Ngwembe,wakati akitoa elimu ya kukabilianan na majanga ya moto kwa wananachi kuelekea  maadhimisho ya siku ya zimamoto Dunia na kusema kuwa vitendo hivyo vinakwamisha juhudi za uokoaji na vinaweza kuhatarisha maisha ,

Sauti ya Mkuu wa Jeshi la zima moto na uokoaji  wilayani Sengerema, Inspekta Juma Ngwembe

Askari wa Jeshi la zima moto na uokoaji Wilayani humo Konstebo Erick Karumuna  amesema changamoto kubwa wanazokumbana nazo ni kupokea simu za uongo,pamoja na kuchezewa simu ya dharura hali inayorudisha nyuma mapambano dhidi ya majanga ya moto.

Sauti ya Askari wa Jeshi la zima moto na uokoaji Konstebo Erick Karumuna

Baadhi ya wananchi wameliomba jeshi hilo kuachukulia hatua kali za kisheria watu wanaochezea simu ya dharura pamoja na kutoa taarifa za uongo za majanga ya moto ili kukomesha tabia hiyo.

Sauti ya baadhi ya wananchi wilayani Sengerema

Aidha maadhimisho ya siku ya Zima moto Duniani yanafanyika Mei 4 mwaka huu   kwa lengo la kuwaheshimu na kuwakumbuka waliopoteza misha wakiwa kazini ,kuthamini mchango wao katika kuokoa maisha na kutoa elimu kwa jamii kuhusu usalama wa moto.