Sengerema FM

Wananchi Buchosa walia na ubovu wa barabara

27 July 2023, 5:10 pm

Picha: Moja ya barabara inayolalamikiwa zaidi na wananchi wa Buchosa Wilayani Sengerema. Picha na Katemi Lenatus

Baadhi ya barabara kongwe nchini zimeonekana kutelekezwa na serikali ili hali zilitumika katika harakati za kudai uhuru wa taifa la Tanganyika zaidi ya miaka 60 iliyo pita.

Na: Katemi Lenatusi

Wananchi wa vijiji vya Busekeseke na Magulukenda katika kata ya  Kalebezo halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza wanalazimika kuuza mazao ya nafaka na mazao ya mbao kwa bei ya hasara  kwa zaidi ya miaka 17 kutokana na miundombinu mibovu ya rabaraba .

Wakizungumza na redio Sengerema kwa nyakati tofauti wananchi wa vijiji hivyo wamesema barabara hiyo inayotoka kijiji cha Kalebezo hadi Mkolani Geita ilikuwa kitovu cha usafirishaji lakini kwa sasa ni zaidi ya miaka 17  imepita barabara haijajengwa hivyo imepelekea shughuri za kiuchumi kukwama katika vijiji hivyo.

Kwa  upande wake diwani wa kata hiyo Isaka Mashimba amekiri kuwepo  kwa ubovu wa barabara hiyo  na  kwamba kwa bajeti ya mwaka 2023/2024 wakala wa barabara za mjini na vijijini TARURA  wilayani Sengerema  imetenga fedha shilingi milioni 200 ambazo zitajenga barabara yenye urefu wa kilometa 10 kutoka  Magulukenda hadi kijiji cha Busekeseke.

Barabara ya Magulukenda hadi Busekeseke na Mkolani Geita licha ya kutokujengwa wala kufanyiwa ukarabati  kwa miaka 17 lakini barabara hiyo itaendelea kukumbukwa kama miongoni mwa barabara zilizotumika kusaka uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.

Sauti ya Mwaandishi wetu Katemi Lenatusi ikifafanua kwa undani zaidi taarifa hii..