Sengerema FM

9 mbaroni mauaji ya kijana aliyeshindwa kulipia pombe Mwanza

12 May 2026, 6:18 pm

Kamanda wa polisi Mkoa wa  Mwanza Wilbroad Mtafungwa akizungumza na wanahabari,Picha na Jeshi la polisi Mwanza.

Kufuatia kukithili kwa watu kujichukulia sheria mkono Jeshila Polisi Mwanza lawakamata watu tisa kwa mauaji.

Na, Emmanuel Twimanye

Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu tisa wakiwemo Mabaunsa wa baa ya Rasvegas kwa tuhuma za mauwaji ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mzafaru Faizar (26) mkazi wa Kata ya Mbugani Jijini Mwanza kwa kushindwa kulipa bili ya shilingi elfu nane  baada ya kunywa pombe.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi Mkoa wa  Mwanza Wilbroad Mtafungwa amethibitisha kutokea tukio hilo.

Sauti ya kamanda wa polisi Mkoa wa  Mwanza Wilbroad Mtafungwa

Kamanda Mtafungwa, amebainisha kuwa baada ya kufanyika kwa tukio hilo jeshi la polisi lilianza kufanya upelelelezi na kufanikiwa kuwakamata  baadhi ya watuhumiwa wa mauaji hayo.

Sauti ya Kamada wa Polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mtafungwa

Aidha, Kamanda Mtafungwa amewataka walinzi wa baa na maeneo ya starehe kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi, na badala yake kuwafikisha watuhumiwa kwenye vyombo vya dola ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Sauti ya Kamada wa Polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mtafungwa