Sengerema FM

Akatwa panga na mpwa wake kisa deni la elfu 80

18 January 2024, 4:47 pm

Mzee Manyema Marco aliye jeruhiwa na mpwa wake kwa kukatwa na panga sehemu mbalimbali za mwili wake akiendelea kupata matibabu katika hospitali teule Sengerema. Picha na Emmanuel Twimanye.

Matukio ya ndugu wa familia kuuana na kujeruhiana kisa mali yamekuwa yakitajwa zaidi nchini ambapo katika wilaya ya sengerema mnamo mwezi October.2023 mtu mmoja aliuwawa na ndugu zake katika kijiji cha Ilunda kata ya Ngoma wakigombania shamba la urithi, Vivyo kwa mzee Manyema Marco ambaye amekatwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake na mtoto wa dada yeke kisa ni kumdai fedha alizomkopesha zenye thamani ya elf.80.

Na;Emmanuel Twimanye.

Mzee mwenye umri wa miaka 61 katika  Mtaa wa  Kizugwangoma  Kata ya misheni Wilayani Sengerema amedaiwa kushambuliwa kwa mapanga  na rungu na kujeruhiwa  sehemu mbalimbali za mwili wake  wakati  akidai deni la shilingi elfu themanini  kwa ndugu yake.  

Akizungumzia tukio hilo mzee huyo aliyefahamika kwa majina ya Manyema Marco amesema kuwa alimkopesha mpwa wake shilingi elfu themanini mwaka jana ambapo alipokwenda nyumbani kwake kumdai ndipo aliposhambuliwa kwa mapanga  na rungu kichwani na miguuni.

Mke wa mzee huyo Skolastica Elias Makanyaga   amesikitishwa na tukio hilo na kushangzawa na kitendo cha ndugu yake kumshambulia  mme wake bila hatia. 

Baadhi ya majirani wa familia hiyo wameiomba serikali kumtafuta mwanaume  aliyedaiwa kumshambulia mzee huyo na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Kizugwangoma Kwiligwa Methusela amethibitisha kutokea kwa tukio hilo  na kuwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi.

Jeshi la Polisi Wilayani Sengerema limefika eneo la tukio na kumchukua mzee aliyeshambuliwa kisha kumpeleka katika Hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema kwa ajili ya kupatiwa matibabu wakati likiendelea kumtafuta mwanaume anayedaiwa kufanya tukio hilo  ambaye ametokomea  kusikojulikana.

Taarifa ya Emmanuel Twimanye inafafanua zaidi