Sengerema FM

Simeo wa Misheni Sengerema akutwa amejinyonga

4 May 2026, 12:31 pm

Baadhi ya waombolezaji,Picha na Emmanuel Twimanye

Changamoto za maisha zatajwa kuwa chanzo cha vijana kujinyonga wilayani Sengerema

Na:Emmanuel Twimanye

Kijana aliyefahamika kwa jina la Simeo Paschal (22) mkazi wa Mtaa wa Misheni Kata ya Misheni, wilayani Sengerema mkoani Mwanza amefariki dunia kwa kujinyonga ,huku chanzo cha tukio hilo kikiwa bado hakijafahamika.

Baadhi ya ndugu wa marehemu pamoja na wakazi wa mtaa huo  wamesikitishwa na tukio hilo na kuwaomba  vijana kuepuka kuchukua maamuzi ya kujitoa uhai pindi wanapokumbana na changamoto za maisha.

Sauti za baadhi ya ndugu na wananvchi

Balozi wa eneo hilo,Safari Merikioli, amelaani vikali tukio hilo na kuwaomba vijana kuwashirikisha watu wa karibu pindi wanapokuwa  na changaoti ili  waweze  kupatiwa ushauri .  

Sauti ya Balozi ,Safari Merikioli

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Misheni, Joseph Protas, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka vijana kuachana na tabia ya kujinyonga .

Sauti ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Misheni, Joseph Protas

Jeshi la Polisi wilayani Sengerema limefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu, kisha kuupeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Sengerema kwa ajili ya taratibu za mazishi.