Sengerema FM

Washauriwa kuepuka mikopo kutoka taasisi zaidi ya moja

5 May 2026, 7:17 pm

Ofsi za kampuni ya kukopesha ya JMS Campany tawi la Sengerema. Picha na Emmanuel Twimanye

Kufuatia kuwepo na malalamiko ya baadhi ya wamama kukimbia miji yao kama njia ya kukwepa kulipa madeni ya mikopo kutoka taasisi za kukopesha maarufu kausha damu, sasa washauriwa kuacha kukopa kwenye taasisi nyingi ili kuepuka fedheha ya kuacha watoto na waume zao.

Na;Emmanuel Twimanye

Wanawake wilayani Sengerema mkoani Mwanza wameaswa kuacha kukopa mikopo kutoka taasisi za kiffedha zaidi ya moja ili kuepuka kukimbia familia kutokana na kushindwa kurejesha mikopo hiyo.

Ushauri huo umetolewa na afisa mikopo kutoka kampuni ya utoaji huduma za mikopo ya fedha ya JMS wilayani Sengerema, Neema Thomas, wakati akitoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi sahihi ya mikopo.

Sauti ya afisa mikopo kampuni ya JMS wilayani Sengerema, Neema Thomas

Bi. Neema amesema ni muhimu kwa wanawake wanaokopa fedha kuhakikisha wanazitumia kwa malengo yaliyokusudiwa, ili ziweze kuwanufaisha kiuchumi na kuboresha maisha yao pamoja na familia zao.

Sauti ya afisa mikopo kampuni ya JMS wilayani Sengerema, Neema Thomas

Kwa upande wao,baadhi ya wanawake wakizungumza kwa nyakato tofauti wameshukuru kwa elimu  hiyo   kwa kuwa kufanya hivyo  kutawasaidia kuepuka kuchukua mikopo kutoka taasisi binafsi zaidi ya moja, jambo ambalo limekuwa likisababisha kushindwa kurejesha na kuathiri familia zao.

Sauti za baadhi ya wanawake wilayani Sengerema wakizungumzia suala la mikopo umiza