Sengerema FM
Sengerema FM
8 May 2026, 6:23 pm

Katika kukabiliana na migogoro ya ardhi Sengerema wananchi zaidi ya 1000 wakabidhiwa hati miliki za kimila
Na,Emmanuel Twimanye
Zaidi ya wananchi elfu moja katika Kijiji cha Ilekanilo, Kata ya Kasungamile, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, wamekabidhiwa hati miliki za kimila, hatua inayolenga kuimarisha umiliki wa ardhi na kupunguza migogoro.
Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa hati hizo, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mh, Senyi Ngaga, amesema hatua hiyo imekuwa suluhisho kwa migogoro ya ardhi, huku akiipongeza kampuni ya upimaji ardhi GMS kwa ushirikiano mzuri.
Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema , Wilfred Mkono, amesema zoezi la upimaji lilianza Februari mwaka huu katika vijiji 16, na tayari vipande 18,639 vimepimwa huku hati 10,307 zikikamilika.
Akizungumza kwa niaba ya wananachi waliokabidhiwa hati hizo Diwani wa Kata ya Kasungamile, Mh, Godfrey Maisa, ameishukuru serikali kwa kuwawezesha kumiliki ardhi zao kisheria.
Mkurugenzi wa GMS Geotech Consultancy Company Limited, Michael Sambu, amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kushiriki zoezi hilo.

