Sengerema FM

Jukwaa la Mwanamke Sengerema lawashika mkono watoto wanaoshi mazingira hatarishi

3 March 2024, 7:29 pm

Mwenyekiti jukwaa wa mwanamke Sengerema Bi. Darine Matonange akikabidhi baadhi ya msaada kwa mmoja wa watoto wanufaika.Picha na Emmanuel Twimanye

Kila mwaka ifikapo tar 08 Machi dunia huadhimisha siku ya mwanamke duniani ambapo hutanguliwa na matukio mbalimbali ambayo hufanywa na wanawake, Jukwaa la mwanamke Sengerema limeanza na kutoa msaada kwa wanafunzi wanaoishi mazingira hatarishi wilayani hapo.

Na;Emmanuel Twimanye

Zaidi ya wanafunzi 100 wanaoishi katika mazingira hatarishi katika shule ya msingi Ibondo wilayani Sengerema wamepatiwa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo madaftari.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa wiki ya  maadhimisho ya  mwanawake duniani  mwenyekiti wa  jukwaa la Mwanawake wilayani Sengerema Bi.Darine Matonange amesema kuwa wanawake wilayani humo  wameguswa kuwasaidia watoto hao ili  wasome katika mazingira rafiki .

Sauti ya mwenyekiti wa  jukwaa la Mwanawake Wilayani Sengerema Bi.Darine Matonange

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ibondo Mwl,Paul Vicent  amesema kuwa jumla ya wanafunzi 124 wanaoishi katika mazingira hatarishi  wamepatiwa msaada huo .

Sauti ya Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ibondo Mwl,Paul Vicent 

Baadhi ya wanafunzi waliopatiwa msaada wamewashukuru jukwaa la  mwanawake Sengerema kwa kutoa  msada huo.

Sauti za baadhi ya wanafunzi Shule ya msingi Ibondo

Naye kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema Yuster Mwambembe  amewataka wanawake kuendelea kupaza sauti dhidi ya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa na waume zao

Sauti ya kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema Yuster Mwambembe 

Aidha siku ya  Mwanawake  Duniani ambayo hufanyika machi 8 kila mwaka, na Mwaka huu  imebebwa na kauli mbiu isemayo “Wekeza kwa wanawake  kuharakisha maendeleo ya Taifa na ustawi wa jamii”.