Sengerema FM
Sengerema FM
16 September 2026, 4:12 pm

Wazazi na walezi wa watoto wenye mahitaji maalumu watakiwa kujua vipaji vya watoto wao mapema ili kuwasaidia kuondoa utegemezi.
Na;Elisha Magege
Jamii imetakiwa kuwapeleka shule watoto wenye mahitaji maalumu ili kuwasaidia kuchangamana na wenzao na kutambua vipaji vyao.
Rai hiyo imetolewa na Mwl. Kahabi Magessa afsa elimu kitengo maalumu msingi na awali katika Halmashauri ya Sengerema wakati akifungua mashindano ya michezo maalumu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu yaliyofanyika Shule ya msingi Sengerema, ambapo amesema mbali na haki yao ya k upata elimu bado watoto wenye mahitaji wanaweza kuwa na vipaji ambavyo kupitia walimu vinaweza kugundulika mapema.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Shirika lisilo kuwa la kiserikali la AWPD Bwn.Sailence Nteko amesema watoto wanabadilika kulingana na mazingira hasa wanapochangamana na watoto wenzao.
Hata hivyo walimu wakuu wa kitengo maalumu shule ya Msingi Sengerema na mkuu wa shule ya Msingi Busisi, wamesema jamii inapaswa kutambua kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wameboresha miundo mbinu ya kujifunzia kwa watoto wenye mahitaji maalumu nchini.
Nao baadhi ya wanafunzi wameishukuru serikali na wadauo shirika la AWPD kwa kuwakutanisha na kufanya michezo mbalimbali, huku wakiwataka wazazi na walezi kuwapeleka shule watoto wenye mahitaji maluumu.
Mashindano ya Special Olpic 2026 yaliyozikutanisha shule za msingi vitengo maalumu Sengerema na Busisi yamefadhiliwa na shirika la AWPD.