Sibuka FM

DC Gidarya: Wananchi wa Ipililo tunzeni huu mradi wa maji

20 March 2025, 1:23 pm

Mkuu wa Wilaya (mwenye skafu shingoni ) Anna Gidarya akipata maelezo kutoka kwa Afisa Maendeleo ya Jamii Ruwasa Wilaya ya Maswa Willlison Magaigwa (aliyeshika mic ) wakati wa kuweka Jiwe la Msingi katika Mradi wa Maji uliopo kijiji cha Ipililo, Kata ya Ipililo, Wilaya ya Maswa, Mkoa wa Simiyu. Picha na Nicholaus Machunda

Baada ya Serikali kujenga Mradi na kuukadhi kwenu, Jukumu la kuulinda na Kuutunza ni lakwenu wananchi wenyewe , hivyo niwaomba wananchi wa Ipililo lindeni miundombinu ya Maji katika Mradi huu, asitokee mwananchi mmoja akaja kukata mabomba halafu nyie mnamuangalia tu. kila mmoja ahusike katika kulinda ” DC Anna Gidarya “

Kaimu  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa     ambaye  ni  Mkuu  wa  Wilaya  Itilima Mkoani  Simiyu  Mhe,   Anna  Gidarya  amewataka  wanachi  wa  Kijiji  cha Ipililo Kata  ya  Ipililo  kuhakikisha  wanatunza  Miundombinu  ya  Maji  katika  Mradi  huo  ili  uendelee  kunufaisha  vizazi   vijavyo.

Mhe  Gidarya   amesema   hayo   wakati  wa  kuweka   Jiwe  la  Msingi  katika  Ujenzi  wa  Mradi   wa  Maji  unaogharimu  zaidi  ya   Bilioni   1. 3   na  kusema  kuwa  suala  la  kutunza  Mradi  ni  jukumu  la  wananchi  mwenyewe.

sauti ya Anna Gidarya akizungumza wakati wa kuweka jiwe la Msingi mradi wa maji Ipililo

Amesema  kuwa   kwa  sasa   Mradi  upo  katika  hatua  za  mwisho  za  Ukamilishaji ,  katika  kipindi  hiki  cha  matazamio  wananchi  wataendelea  kuchota  maji  bure  huku  akiwapongeza   Ruwasa   wilaya  ya  Maswa  kwa  Usimamizi  Mzuri  wa  Mradi  huo  unaoenda  kumtua  mama  ndoo  kichwani.

sauti ya Anna Gidarya akizungumza wakati wa kuweka jiwe la Msingi mradi wa maji Ipililo
muonekano wa tanki la Maji katika Mradi wa Maji Ipililo

Akitoa   taarifa  kwa   Mgeni  rasmi,  kaimu  meneja  wa   wakala  wa  Maji  na  Usafi  wa  Mazingira  Vijijini (ruwasa )  wilayani Maswa  Mhandisi   Jofrey   Kiama  amesema  kuwa   lengo  la Mradi ni  kutoa  huduma  ya  Maji  kwa  wananchi  wa  Ipililo  huku  akisema ushirikishwaji  wa  jamii  ukiwa  umezingatiwa.

sauti ya Eng, Jofrey Kiama Kaimu meneja Ruwasa Maswa akitoa taarifa ya mradi kwa mgeni rasmi

Akizungumza  kwa  niaba  ya   Mbunge  wa  Jimbo  Maswa  Mashariki   katibu  wa  Mbunge  huyo   Ndugu  Marco   Bukwimba  amesema  suala  la  Maji  katika  kijiji  cha  Ipililo  lilikuwa  linamnyima  Usingizi  lakini  kwa  sasa   ameutua  huo  mzigo  aliokuwa  ameubeba  kwa  Muda  mrefu   Mhe  Mbunge  Stanslaus Nyongo.

sauti ya Marco Bukwimba Mwakilishi wa Mbunge Jimbo la Maswa Mashariki

Diwani  wa  Viti maalumu  ccm  kata  ya  Ipililo   Mhe  Modester  Mussa   Kabeya   kwa  niaba  ya  wananchi  wa  Ipililo  amemshukuru  Rais  wa  Jamhuri  ya  Muuungano  wa  Tanzania  Mhe  Dkt  Samia  Suluhu  Hassani  kwa  kutoa  Fedha  ili  kujenga  Mradi  wa  Maji  katika  kijiji  hicho  kwani   wananchi walikuwa  wakipata   adha  kubwa   ya  kuamka  Usiku  kwenda  kutafuta  Maji

sauti ya Modester Diwani viti maalum na baadhi ya wananchi wa Ipililo
baadhi ya wananchi wa kijiji cha Ipililo wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya wakati wa uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa maji Ipililo