Sibuka FM

RC Macha ataka elimu ya matumizi ya barabara

17 March 2026, 6:19 am

Pichani ni mkuu wa mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha akiwa kwenye mojawapo ya shughuli za kila siku za kiserikali akizungumza jambo na wajumbe wa kikao. Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Anamringi Macha ameagiza watu wote wanoharibu miundombinu ya barabara kwa namna mbalimbali ikiwemo kupitisha mifugo kwenye barabara za lami mkoani humo wapatiwe elimu juu ya matumizi ya barabara na baada ya kuelemishwa wale wote watakaoendelea kufanya shughuli zinazoharibu miundombinu hiyo wachukuliwe hatua”.

Na,Daniel Manyanga 

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha ameziagiza mamlaka za barabara  tutoa elimu ya matumizi ya miundombinu hiyo kabla ya kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu wanaoharibu barabara kupitia shughuli mbalimbali wanazofanya kama kupitisha Mifugo kwenye lami.

Anamringi Macha ametoa maagizo hayo  wakati akizungumza katika kikao cha bodi ya barabara mkoani hapo ambapo amesema kuwa kuna kila haja kwa mamlaka kutoa elimu ya matumizi ya barabara za lami hasa kwa wananchi na kutokana na jamii kubwa mkoani hapo kujihusisha na ufugaji hivyo kupitisha mifugo yao kwenye lami.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha

Awali akizungumza katika kikao hicho meneja wa wakala wa barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Simiyu mhandisi Boniphace Mkumbo ameeleza jitihada mbalimbali wanazozifanya kukarabati barabara zilizoharibika.

Sauti ya meneja wa TANROADS mkoa wa Simiyu, Boniphace Mkumbo
Pichani ni mkuu wa wilaya ya Maswa,Dkt.Vicent Naano Anney mmoja wapo wa wajumbe akichangia hoja juu ya ubovu wa barabara na namna ya kuzitengeneza Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Kwa upande wao baadhi ya wajumbe wa kikao hicho ,Vumi Magoti,Masunga Mizingo na Vicent Anney  wakaeleza changamoto za ubovu wa barabara katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Simiyu huku wakiomba zifanyiwe matengenezo ili kurahisisha usafiri hasa kwa watumiaji wa miundombinu hiyo.

Sauti ya wajumbe wa kikao hicho cha RCC