Sibuka FM

DC Anney atangaza msako kwa wadaiwa sugu wa mikopo ya 10%

11 March 2026, 2:21 pm

Pichani ni mkuu wa wilaya ya Maswa ,Dkt.Vicent Naano Anney akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mikopo kwa wajasiriamali katika makundi ya vijana,wanawake na watu wenye ulemavu Picha na Samwel Mwanga

Hatuwezi kupoteza fedha za walipa kodi kwa watu wasiokuwa waaminifu wanaokuja kwa kuomba mikopo kwenye halmashauri zetu wanapewa ikifika wakati wa marejesho wanaingia mitini lazima tuwe na sheria kali katika kulinda kodi za wananchi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.”

Na,Daniel Manyanga 

Mkuu wa wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, Dkt.Vicent Naano Anney amevitaka vyombo vya sheria kuwafikisha mahakamani wale wote walipata mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya ndani ya halmashauri na kushindwa kurejesha kwa wakati ili kuwapatia fursa vikundi vingine kupata mikopo hiyo.

Pichani ni afisa maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Maswa, Hollo Ngeme akizungumza na vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu walipewa mikopo ya kujikwamuwa kiuchumi mikopo hiyo itokanayo na mapato ya ndani ya asilimia kumi Picha na Samwel Mwanga

Dkt.Annery amesema kuwa kuna vikundi vilipata mikopo hiyo kwa lengo la kujiinua kiuchumi kutokana na shughuli wanazozifanya lakini mpaka sasa hivi havijarudisha mikopo hiyo kwa ajili ya kuwapatia wengine mikopo huku zaidi milioni mia saba ikiwa mikononi mwa watu wasiokuwa waaminifu katika kurejesha mikopo isiyokuwa na riba.

Mkuu huyo ameongeza kuwa haiwezekani watu wachache wakope kwa lengo la kujiinua kiuchumi halafu ikifika wakati wa kurudisha wanatokomea kwingine bila kurejesha hivyo hatua kali za kisheria zichukuliwe kwa vikundi ambavyo havijarejesha mikopo ikiwemo kuwaburuza mahakamani kama sheria inavyosema.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa, Dkt.Vicent Naano Anney
Picha katika matukio mbalimbali wakati wa semina elekezi kwa vikundi vilivyoweza kupata mkopo wa asilimia kumi ya mapato ya ndani ya halmashauri hiyo Picha na Samwel Mwanga