Sibuka FM
Sibuka FM
24 February 2026, 8:52 am

Mimi nataka kuwa mkweli kama mpango wako wa kulima pamba ili upate kilo mia tatu (300) kwenye hekari moja afadhali nenda ukafanye kazi nyingine maana utakuwa unajitafutia umasikini ” RC Simiyu Anamringi Macha”
Na Nicholaus Machunda
Wakulima wa zao la pamba Mkoani Simiyu wameshauliwa kufuata kanuni bora za kilimo cha zao hilo ili kuleta tija na kujikwamua kiuchumi kwa kuzalisha pamba nyingi.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe Anamringi Macha kwenye mkutano Mkuu wa nane(8) wa Chama kikuu cha ushirika SIMCU 2018 LTD Uliofanyika wilayani Maswa
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa,amewasisitiza wakulima kulima kilimo cha kisasa cha kufuata kanuni za kilimo na ushauri wa watalaamu badala ya kulima kilimo cha mazoea kinachowaletea umasikini na kusababisha hasara
Kwa upande wake, Bi, Consolata Kiluma ambaye ni naibu mrajisi wa vyama vya ushirika nchini amewaeleza wajumbe wa bodi ya vyama vya ushirika kuwa waadilifu katika kutekeleza majukumu yao ili kuleta ufanisi katika Ushirika

Naye Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Simiyu, Ndugu Godfrey Mpepo amesema kuwa ushirika uko vizuri tangu kilipoanzishwa chama kikuu cha ushirika Mkoa wa Simiyu SIMCU Ltd
