Sibuka FM
Sibuka FM
19 February 2026, 1:03 pm

“Kuna wilaya zingine hazina hata gari la zimamoto la kisasa kama hili lenye uwezo mkubwa wa kubeba tani tano lakini sisi tumepata lazima sasa hapo tukatunze sana huo mtambo ili uwasaidie wananchi pale ambapo panapotokea changamoto ya moto tuweze kuzima ili kuzuia madhara kwa wananchi.”
Na,Daniel Manyanga
Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Anamringi Macha amelitaka jeshi la zimamoto na uokoaji mkoaa hapo kulitunza gari jipya la zimamoto lililokabidhiwa kwa jeshi la zimamoto na uokoaji wilayani Maswa ili liweze kufanya kazi iliyokusudiwa na serikali hususani majanga ya moto yanapotokea katika kuzima ikiwa ni mtambo wa kwanza tangu uwepo wa wilaya hiyo kongwe yenye zaidi ya miaka 100 ambapo mtambo huo umegharimu shilingi bilioni 1.3.

Anamringi Macha ametoa maagizo hayo wakati wa kukabidhi mtambo huo kwa jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Maswa na kuongeza kuwa ni vyema mtambo huo ukatunzwa ili kuweza kuwahudumia wananchi katika kukabiliana na majanga ya moto pamoja na kuhakikisha kwa mamlaka zinazohusika na miundombinu ya barabara hasa vijijini zinakarabati miundombinu hiyo ili kuwezesha gari hilo liweze kupita bila shida yoyote.
Wakizungumza na kipindi hichi baada ya makabidhiano hayo baadhi ya wananchi walioshuhudia hafla hiyo,Suzana Shindah,Benard Mgindi na Yunisi Sayuni wamesema kabla ya ujio wa mtambo huo walikuwa wakitumia mbinu za kiasili ikiwa ni pamoja na kutumia mchanga, kupiga yowe ili kukusanya watu kusaidia kuzima moto hivyo kuishia kupata hasara ya kuunguliwa na vitu vyote kutokana na mbinu duni za kuzimia moto.

Kwa upande wake kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Simiyu, ASF Faustin Mtitu na mbunge wa jimbo la Maswa mashariki, Dkt.George Lugomela wamesema kuwa mtambo utasaidia sana katika kuzima moto pale ambapo ikitokea kutokana na mtambo huo kuwa na uzito mkubwa kwa ujazo wa maji pekee kg 5,000 sawa na tani tano hivyo uhitaji wa barabara za uhakika ikiwa ni sambamba na kuhitaji maji ya uhakika.