Sibuka FM
Sibuka FM
16 February 2026, 1:14 pm

“Kwani sheria zetu zipo kwa ajili ya kumuhukumu nani kama kuna watu hadi leo wanatumia vibaya mamlaka na utajiri wao kuwaumiza wananchi wengine ambao hata hawana wanalolijuwa juu ya utajiri wako .”
Na,Daniel Manyanga
Hali ya wasiwasi na hofu kubwa imetanda kwa wakazi wa kata ya Isanga wilayani Bariadi mkoani Simiyu kufuatia kiwanda cha kuchakata pamba na alizeti kutiririsha maji machafu yanayodaiwa kuwa na kemikali hivyo wameiomba serikali kuingilia kati na kuchukua hatua za haraka ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.
Wakizungumza na Sibuka Fm baadhi ya wakazi hao, Mawazo Lyangala, Sitta Sayi, Paulo Lucas na Singu Ngimba wameeleza athari walizozipata hadi sasa kutokana na maji hayo ya kiwandani kutiririshwa kwenye maeneo yao.
Sitta Masunga ni Mwenyekiti wa mtaa wa Katenga na Nashoni Ngusa ambaye ni diwani wa kata Isanga wameleeza kuwa maji hayo hadi sasa yameathiri mifugo, maeneo pamoja na mazao mbalimbali yaliyopo shambani.
Kwa upande wake Monica Deusdedith ambaye ni afisa mazingira wa halmashauri ya mji wa Bariadi na Nkenyenge Charles Nkenyenge ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Bariadi wanaeleza hatua walizozichukua dhidi ya uongozi wa kiwanda hicho hadi sasa ili kukomesha tatizo hilo.