Sibuka FM

Zaidi bilioni 39 zapitishwa kwa matumizi mwaka wa fedha 2026/27 Bariadi DC

13 February 2026, 12:52 pm

Picha ya pamoja ikiwaonesha madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Bariadi wakiwa katika kikao cha baraza la madiwani wakati wakujadili bajeti Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Hatutakuwa na uvumilivu kwa watendaji wazembe ambao watakuwa sehemu ya kukwamisha ukusanyaji wa mapato ya halmashauri tunataka ufanisi zaidi katika kukusanya mapato ili kurahisisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi”.

Na,Daniel Manyanga 

Baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu limepitisha mapendekezo ya bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 39 katika mwaka wa fedha 2026/27 kama matumizi ya utekelezaji wa shughuli za miradi ya maendeleo, matumizi ya kawaida na mishahara katika halmashauri hiyo.

Akizungumza na Sibuka Fm katika kikao cha baraza la madiwani mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Mayala Lucas amesema baraza limepitisha  bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 39 katika mwaka wa fedha 2026/27 huku watumishi wakikumbushwa kusimamia ukusanyaji wa mapato ili kufikia malengo ya halmashauri iliyojiwekea.

Sauti ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bariadi, Mayala Lucas

Awali akizungumza katika kikao hicho kaimu mkuu wa idara ya mipango wa halmashauri hiyo, Sayi Luseba ametoa mchanganuo wa bajeti hiyo, huku kaimu mkurugenzi wa hamlashauri hiyo, Albert Siogopi amesema kuwa watahakikisha wanasimamia ukusanyaji wa mapato kwa ufanisi mkubwa.

Sauti ya kaimu mipango na kaimu mkurugenzi

Kwa upande wao baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo akiwemo,Deogratius Mayala, Emmanuel Maseko na Charles Lyaganda, wameeleza walivyojipanga kusimamia suala la ukusanyaji wa mapato ili kufikia malengo yaliyowekwa na halmashauri ya wilaya ya Bariadi.

Sauti ya madiwani wakieleza utayari wao katika kusimamia ukusanyaji wa mapato katika maeneo yao ya kiutawala