Sibuka FM

Hospitali ya BARIKIWA yaleta burudani kwa wakazi wa Maswa

15 December 2025, 10:22 pm

Wachezaji wa timu ya Rhino rangers ya Tabora wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Hospitali ya Barikiwa iliyopo mjini maswa Dr Ashley Lucas (mwenye tisheti nyeusi mbele ) baada ya wachezaji hao kutembelea kituo hicho kabla ya kuanza mchezo. Picha Na Nicholaus Machunda

Kwa sasa mpira ni ajira hivyo vijana mcheze kwa malengo kwa kujituma na nidhamu ili mfikie malengo yenu ya kucheza mbali zaidi, Lakini pia nikupongeze sana Mkurugenzi wa Hospitali ya Barikiwa kwa kutekeleza azma ya serikiali kuhusu Ushirikiano na sekta binafsi. ” Athuman Kalaghe -katibu tawala wilaya ya Maswa “

Kituo cha  afya  cha  Barikiwa  kilichopo  wilayani  Maswa  Mkoani  Simiyu  kimekutanisha wananchi  wa Wilaya  hiyo  kwa  kuleta  mchezo wa kirafiki  wa  Mpira  wa  Miguu  kati ya   Rhino Rangers ya  Tabora  na  Barikiwa  Maswa star ya  mjini  maswa  mchezo uliochezwa  katika  uwanja  wa  ccm  nguzo nane.

Akizungumza  wakati wa ufunguzi  wa  mchezo  huo, katibu tawala  wilaya  ya  Maswa  ndugu   Athuman  Kalaghe  ambae  alikuwa  mgeni  rasmi  amesema  kuwa kwa sasa michezo  ni  ajira  lakini pia  inakutanisha  watu  mbalimbali  huku  akipongeza  Uongozi wa  Kituo cha  afya Barikiwa  kwa kuunga mkono azma  ya  Serikali ya  kushirikiana na sekta binafsi   ili kuleta  maendeleo.

sauti ya Athuman Kalaghe- DAS Maswa akizungumza na wachezaji
Athuman Kalaghe- DAS Maswa akisalimiana na wachezaji wa Rhino rangers

Kwa  upande  wake  Mkurugenzi  wa  Kituo cha  Afya  Barikiwa  Dr  Ashley Lucas  amesema  kuwa  lengo la mchezo huo ni  kutengeneza  ujirani mwema  na  kusongeza  burudani  kwa  wananchi wa  Maswa  huku  akisema  michezo ni  sehemu  ya  afya  hivyo anashukuru uongozi wa  timu ya  Rhino rangers  kwa  kukubali  kuja  kucheza   hapa maswa

sauti ya Dr Ashley Lucas- Murugenzi wa Hospitali ya Barikiwa akizungumzia mchezo

Aidha  Dr  Ashley  amesema  kuwa  kabla  ya mchezo  huo  wachezaji  wa  timu ya  Rhino rangers  walipata  nafasi ya  utembelea  kituo hicho cha  Barikiwa   na  kujioneo  huduma  zinazotolewa  pamoja  na  vifaa  vya  kisasa  kabsa  kwa  ajili ya  kusogeza  huduma kwa  wananchi  huku  akitaja  huduma zinazopatikana  hapo.

sauti ya Dr Ashley Lucas- Murugenzi wa Hospitali ya Barikiwa akizungumzia huduma
baadhi ya Vifaa vya kisasa vinavyopatikana Hospitali ya Barikiwa

Alex   Male  ni  kiongozi  wa  msafara  wa  timu ya  Rhino rangers  ameipongeza  Hospitali ya  Barikiwa  kwa  kuwaalika  kuja  kucheza mechi ya  kirafiki na  kusema  timu ya  barikiwa  Maswa star  ni  nzuri   inahitaji marekebisho  madogo  ili kufikia  kiwango cha  juu  zaidi

sauti ya Alex Male kiongozi wa msafara wa timu wa Rhino rangers

Katika  mchezo huo wa  kirafiki  ulihudhuriwa na  wadau mbalimbali na  wapenda  michezo  kutoka  viunga vya  mji  wa  maswa   ambapo  matokeo katika  mchezo  huo  wageni  Rhino  rangers kutoka  Tabora  walishinda  magori  2  na Vijana  wa   Barikiwa  Maswa  star  wakipata  gori 1

viongozi na wachezaji wa timu ya Rhino wakipata maelezo ya namna ya kitanda cha kutunza watoto wanaozaliwa chini ya Umri (Njiti )kutoka kwa Daktari wa Hospitali ya Barikiwa
Viongozi wa kituo cha afya Barikiwa wakisalimiana na wachezaji wa Rhino rangers