Sibuka FM

Zaidi ya milioni 156 zimetolewa kwa wajasiliamali Itilima

23 October 2025, 5:10 pm

Pichani ni mkuu wa wilaya ya Itilima, Anna Gidarya akizungumza jambo kwenye moja wapo wa shughuli ya kiserikali iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya

Tunataka kuwa na wananchi wenye uchumi himilivu katika taifa hili ili kusaidia kupunguza umasikini uliokithili,kupunguza vifo vitokanavyo na watu kukosa pesa ya kujikimu kimatibabu ikuwa pamoja na kuondoa changamoto ya wimbi la watoto mitaani”. 

Na,Daniel Manyanga 

Zaidi ya milioni 156 zitokanazo na mapato ya ndani ya halmashauri katika wilaya ya Itilima mkoani Simiyu zimetolewa kama mkopo wa asilimia 10% kwa wanufaikaji 125  kwenye vikundi  vya Wanawake,Vijana na Watu wenye ulemavu ili kuwainua kiuchumi katika shughuli wanazofanya.

Wakizungumza na Sibuka Fm baadhi ya wanufaikaji  wa mikopo hiyo katika kundi la Vijana ,Wanawake na watu wenye ulemavu wanasema kipindi cha nyuma ambapo mikopo hiyo ilisitishwa walipata changamoto ya kupata mitaji ya kuendesha shughuli zao za ujasiliamali.

Sauti ya baadhi ya wanufaikaji wa mikopo hiyo wakielezea namna ambavyo wataenda kujikwamua kiuchumi

Jonathan Buluba ni kaimu afisa maendeleo ya jamii wilaya ya Itima amesema vikundi vilivyopewa mikopo ni vile vilivyokidhi vigezo  huku  Irene Masaki meneja mahusiano mwandamizi biashara za serikali kutoka benki ya NMB akiwaomba wale wote waliopata mikopo kuitumia  kwa nidhamu na malengo yaliyokusudiwa.

Sauti ya afisa maendeleo ya jamii na meneja uhusiano na biashara wa NMB wakiwataka wakopaji hao kuzitumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Itilima, Anna Gidarya  amewataka wanufaikaji wa mikopo hiyo ya asilimia kumi ya mapato ya ndani ya halmashauri  kurejesha kwa wakati ili kukidhi vigezo vya kukopesheka kwa mara nyingine ikiwa ni sambamba na kuongeza wigo wa makundi mengine kukopesheka.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Itilima, Anna Gidarya akiwaomba wanufaikaji wa mikopo hiyo kuitumia mikopo kwa lengo lililokusudiwa