Sibuka FM

DC Maswa wezi wa vifaa vya trekta kupandishwa kotini

20 October 2025, 9:02 pm

Kwenye picha ni muonekano wa baadhi ya trekta zilizokabidhiwa kwa wakulima ili kuongeza uzalishaji wa pamba Picha na Samwel Mwanga

Kuna misemo huko mtaani kuwa mali ya serikali haina mwenyewe nataka kuwaambia kuwa haya matrekta mwenyewe yupo ukifanya unavyojuwa wewe tutakuchukulia hatua kali za kisheria”. 

Na,Daniel Manyanga 

Mkuu wa wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu, Dkt.Vicent Naano Anney ameitaka bodi Pamba nchini wilayani hapo kutowapa matrekta wale wote walioharibu na kuchelewa kuwalimia wakulima wa zao pamba katika msimu wa mwaka jana wa kilimo tunapoenda kuanza msimu mpya wa mwaka 2025/2026.

Dkt.Anney ametoa maagizo hayo kwa bodi ya Pamba wakati akikabidhi trekta 50 zilizotolewa na serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania katika kukuza sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji wa pamba pamoja na kupata tija kwa wakulima hao.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa akiitaja bodi ya pamba kutowapatia trekta walioharibu msimu uliopita
Pichani ni mkuu wa wilaya ya Maswa,Dkt.Vicent Anney akitoa maelekezo kwa wakulima pamoja na bodi ya pamba katika kusimamia trekta hizo Picha na Samwel Mwanga

Dkt.Anney ameitaka bodi hiyo kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wote watakaobainika kuiba vifaa (Spea) za trekta kutokana matukio ya mwaka jana watu kuiba spea hizo na kuuza kwingine.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa akitoa onyo kwa wezi wa vifaa

Kwa upande wake mwakilishi wa bodi ya pamba wilaya ya Maswa,Ally Mabrouk  amesema msimu wa kilimo cha zao la pamba 2025/2026 umeanza na wametekeleza jukumu la kuwahudumia wakulima katika ulimaji na matrekta hayo yaingie mashambani.

Sauti ya Ally Mabrouk mwakilishi wa bodi ya pamba wilaya ya Maswa

Nao baadhi ya madereva wa matrekta hayo wakawa na haya ya kusema.

Sauti ya dereva akizungumza namna ambavyo ataenda kusimamia trekta hilo