Sibuka FM

Wenyeviti vitongoji, vijiji Maswa wapigwa msasa

2 September 2025, 5:21 pm

Picha aliyesimama ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Dkt Vicent Naano Anney akizungumza na Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji ( hawapo pichani ) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea Uelewa katika usimamizi wa miradi ya maendeleo. Picha na Nicholaus Machunda

Nendeni mkasimamie shughuli za maendeleo kwenye vijiji vyenu, muone uchungu wa fedha za miradi zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo, mzuie wizi wa fedha na vifaa kwenye Miradi ya maendeleo ” DC Maswa Dkt Vicent Anney ”

Wenyeviti  wa  Vitongoji  na  Vijiji katika  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Mkoa  wa  Simiyu  wamepewa  mafunzo  kwa  ajili  ya kuwajengea  uwezo  katika  kutekeleza  majukumu  yao  na usimamizi  wa  Miradi  ya  maendeleo .

Akifungua  mafunzo  hayo Mkuu  wa  Wilaya ya  Maswa  Mhe,  Dkt  Vicent   Naano  Anney   amewataka wenyeviti  hao  kwenda  kusimamia  miradi  ya  maendeleo  ili  kukuza  uchumi  wa  Wilaya  na  mtu  mmoja  mmoja

sauti ya Dc Maswa Mhe, Vicent Anney akizungumza na wenyeviti wa vitongoji na vijiji

Mhe,  Dkt  Anney  amesema kuwa  mafunzo  hayo  ni  muhimu  kwani  maendeleo  na  mipango  yote  inatoka  kwa  wananchi  ambao  wenyeviti  wa  Vijiji  na  vitongoji  ndio wasimamizi  katika  maeneo  hayo hivyo  ni  watu  muhimu kwa Dira  ya  maendeleo ya  Vijiji

sauti ya Dc Maswa Mhe, Vicent Anney akizungumza na wenyeviti wa vitongoji na vijiji
Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakifuatilia mafunzo

Akimkaribisha  Mkuu  wa  Wilaya katika Ufunguzi wa  Mafunzo hayo,  Mkurugenzi  Mtendaji  Halmashauri ya Wilaya  ya  Maswa  ndugu Maisha  Mtipa  amesema  kuwa wameshirikiana na chuo cha  Serikali  za  mita  Hombolo Dodoma kutoa elimu kwa Wenyeviti hao  ili  waweze kujua  majukumu  pamoja  na taratibu za  uendeshaji  wa  shughuli za  Serikali

Sauti ya DED Maswa ndugu Maisha Mtipa akizungumza wakati wa mafunzo

Ismail  Juma  Kalunde  ni  Mhadhiri  katika  Chuo cha  Serikali  za  Mitaa  Dodoma (Hombolo)  amesema kuwa wenyeviti  hao ndio  wasimamizi  wakuu  katika  miradi  ya maendeleo  hivyo  wanawapa  uelewa  wa  sheria  zinazounda  Mamlaka  za  Serikali  za  Mitaa  pamoja  na  manunuzi  katika mamlaka hizo.

Sauti ya Ismail Kalunde Mhadhiri chuo cha Serikali za Mitaa- Dodoma

Baadhi  ya  wenyeviti wa Vitongoji na  Vijiji  walioshiriki  mafunzo  hayo wameishukuru  Serikali  kwa  kuwapatia mafunzo  kwani  yataenda  kuwakumbusha  majukumu  yao  na  mambo  wanayotakiwa  kufanya  kwa  wananchi  ikiwemo  usimamizi  wa  miradi  ya  maendeleo

sauti za baadhi ya Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji waliopata mafunzo
Picha za matukio katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa