Sibuka FM

Maswa yazindua chanjo ya mifugo, DC Anney atoa maagizo

31 August 2025, 10:39 am

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Vicent Naano Anney akizindua zoezi la chanjo ya Mifugo katika kijiji cha Mwanhegele, kata ya nyabubinza wilaya ya Maswa, Picha na Nicholaus Machunda

Zoezi la chanjo ya mifugo siyo la hiari bali la lazima maana lipo kisheria na linasaidia kupunguza magonjwa ya mlipo kwa mifugo hivyo wafugaji wote muone umuhimu wa zoezi hili kwa kuipeleka mifugo yenu ikapate chanjo” DC Maswa Dkt. Vicent Anney

Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Mkoa  wa  Simiyu imezindua chanjo ya mifugo kwa ajili  ya  kukinga  mifugo  dhidi  ya  magonjwa  mbalimbali ikiwemo homa ya mapafu kwa ng’ombe

Akizindua  zoezi  la  chanjo  hiyo, Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mhe  Dkt  Vicent  Naano  Anney amesema  lazima  zoezi hili  lisimamiwe vema ili mifugo yote ichanjwe kwani ni lazima wala siyo hiari

DC Maswa Dkt Vicent Anney akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanjo ya mifugo

Mhe  Anney  amewashauri  wafugaji kutafuta  mbegu  bora  za  mifugo  ili kuleta  ushindani  katika  soko la  nyama  nje  ya  nchi na  kuongeza  uchumi na  tija  kwa  wafugaji  huku  akiagiza wataokaidi kuchanja  mifugo  yao  wapelekwe Mahakamani  kwa  hatua za  kisheria  

Sauti ya Dc Maswa Dkt Vicent Anney akizungumza wakati wa Uzinduzi wa chanjo ya mifugo

Charles  Msira  ni  Daktari  wa  Mifugo katika  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  amesema  ametaja idadi ya  mifugo  na malengo waliyojiwekea  katika  kufanikisha  zoezi  hilo  la  uchanjaji wa  mifugo

Sauti ya Charles Msira daktari wa mifugo Maswa akitoa taarifa kwa mgeni rasmi

Msira  amesema  kuwa  chanjo  hii  ni  muhimu  kwa  mifugo  kwani  itaenda kudhibiti milipuko  ya  magonjwa  ya  mifugo, kuongeza  uzalishaji wa  mazao ya  mifugo yenye  ubora  na  salama  kwa  watumiaji  huku akitaja  hasara  za  kutochanja  mifugo.

Sauti ya Charles Msira – daktari wa mifugo Maswa akitoa taarifa kwa mgeni rasmi

Nao  baadhi  ya  wafugaji wa  kata ya  Nyabubinza  wakaelezea  furaha  yao baada  ya  kuletewa huduma  ya  chanjo  kwa  hapo  awali  walikuwa  wanapoteza  mifugo  kutokana  na  magonjwa mbalimbali  na  kutumia  fedha  nyingi  kutibu mifugo  yao

Sauti za baadhi ya wafugaji wakiishukuru Serikali kwa kuleta chanjo ya mifugo
Picha za matukio ya zoezi la uchanjaji wa mifugo