Sibuka FM

Waraghbishi Maswa wajengewa uwezo ushiriki wa shughuli za maendeleo

26 August 2025, 12:06 pm

Picha (aliyesimama) Richard Temu -Mraghbishi kutoka shirika la twaweza akitoa mada kwa waraghbishi walioshiriki mafunz katika Ukumbi wa Ndemax -Maswa Picha na Nicholaus Machunda

Uraghbishi siyo mradi, Uraghbishi ni Maisha ya kila siku yakubadilisha fikira na mitazamo ya Jamii katika ushiriki na utatuzi wa changamoto zinazowakabili katika Jamii maana hamna siku changamoto zitaisha katika hivyo wananchi wawe na uwezo wa kuzitatua wao wenyewe, lengo ni kupunguza utegemezi wa wananchi kwa Serikali na kuongeza ushiriki wa shughuli za maendeleo-” Marius Isavika -Kasodefo

Zaidi  ya  Waraghbishi  40   Wilayani  Maswa  Mkoani  Simiyu wamepewa  mafunzo ya  kuwajengea  uwezo  wa  kushiriki  katika  miradi  mbalimbali ya  maendeleo  katika  Jamii  zao

Mafunzo  hayo  yaliyoandaliwa  na  Shirika  la  Kawiye Social Development Foundation (Kasodefo) kwa kushirikiana  na  Shirika la  Twaweza   yakiwa na  lengo kuamsha  ari  ya   jamii   katika  kupanga , kuibua  na  kushiriki  utekelezaji  wa  vipaombele  vya maendeleo katika  Jamii  zao.

sauti ya Richard Temu- mraghbishi kutoka shirika la twaweza

Marius  Isavika  ni  Mratibu  kutoka  Shirika  la  Kasodefo  amesema  kuwa  mafunzo  hayo yataenda  kuondoa  utegemezi  wa  wananchi  kwa  Serikali, kuongeza  ushiriki  katika  masula ya  maendeleo   pamoja  na  kuongeza  uwajibikaji

sauti ya Marius Isavika kutoka shirika la Kasodefo

Aidha  Isavika  ameongeza  kuwa  wamewajengea  uwezo  wa kutumia  vyombo  vya  habari  na Teknolojia  ya  habari  katika  kutangaza  kazi za  Uraghbishi  ili kufikia  watu  wengine   zaidi

sauti ya Marius Isavika -Kasodefo
Picha aliyesimama (mwenye suti ) Marius Isavika kutoka shirika la Kasodefo akizungumza na waraghbishi

Baadhi  ya  washiriki  wa mafunzo  hayo  wameeleza  namna  wanavyoshirikiana  na  viongozi  wa  Serikali  ya  Kijiji  na  Wananchi  katika  Kuibua, Kupanga na  kushiriki  namna  ya  kutatua  changamoto zinazowakabili  katika  maeneo  yao

sauti za baadhi ya waraghbishi wakizungumza baada ya kupata mafunzo
Picha ni washiriki wa mafunzo wakifuatilia mada zilizokuwa zinawasilishwa na wakufunzi