Sibuka FM

CHAUMMA yaeleza mikakati kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 2025

14 August 2025, 5:26 pm

Gimbi Masaba Mratibu wa Uchaguzi chama cha chaumma kanda ya Serengeti akizungumza katika Mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika viwanja vya madeco Wilayani Maswa Pichana na Nicholaus Machunda

Chama cha Ukombozi wa Umma siyo chama kigeni, ni chama kikongwe ila kilikuwa kinatambulika zaidi ngazi za Juu lakini kwa sasa tumeamua kukishusha ngazi za chini kabisa kwa wananchi wakitambue na kukipa ridhaa “Gimbi Masaba -Mratibu wa Uchaguzi Chaumma kanda ya Serengeti “

Chama  cha  ukombozi  wa  Umma (chaumma )  kimesema kuwa  imejipanga  kikamilifu  kushiriki  Uchaguzi  mkuu  wa  Rais ,  Wabunge  na  Madiwani  utaofanyika  mwishoni mwa mwezi  Oktoba  mwaka  2025  huku  sera  yake  ikiwa  ni  kuimarisha  Afya  na  Lishe  kwa   Watanzania

Hayo  yamesemwa  na  mratibu  wa  uchaguzi  chaumma  kanda  ya  Serengeti  Bi  Gimbi  Dotto  Masaba   wakati  wa  Ziara  ya kutambulisha  chama  hicho  kwa wananchi  wa  Maswa  Mkoani  Simiyu  huku  akiomba  watanzania  na  wana  Maswa  kukiunga  mkono  ili kiweze kuleta  Ukombozi  kwa  wananchi

sauti ya Gimbi Masaba akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini maswa

Masaba  amesema  kuwa  wameamua  kutoka  chadema  na  kujiunga  na  chaumma   ili  washiriki  uchaguzi  mkuuu   na  kudai mabadiliko  wakiwa  na   wawakilishi  katika   ngazi  za  maamuzi  ikiwemo   Bungeni  huku  akisema  Vijana  wengi  wamejitokeza  kuchukua  fomu ili  waweze  kuleta  mabadiliko

sauti ya Gimbi Masaba
Gimbi Masaba aliyeshika Mic akiwatambulisha watia nia udiwani kupitia chama cha Chaumma

Kwa  upande  wake  mratibu  wa  uchaguzi   Mkoa  wa  Simiyu  Bi  Kwandu  Mpanduzi  amesema  kuwa chaumma  kimedhamilia  kwenda  kutetea  wakulima  hasa  wa  zao  la  pamba  ambalo  limekuwa  na kizungumkuti  na  manyanyaso  kwa  wakulima kutokana  na  zao  hilo  kufanywa  na  Wabunge  ambao  ndio   watunga  sera

sauti ya Kwandu Mpanduzi mratibu wa uchaguzi chaumma mkoa wa Simiyu

Flora  Masuke  na  James  Mahangi  ni  watia  nia  wa  Ubunge  jimbo  la  Maswa  mashariki  kupitia  chama  cha  Chaumma wameahidi  kuleta  Mabadiliko  kwa  Maswa  endapo  wananchi   wataunga  mkono  na  kuwachagua

sauti ya Flora Masuke na James Mahangi watia nia Ubunge kupiti chama cha Chaumma