Sibuka FM

Wakiukaji sheria za uuzaji wa dawa muhimu wakalia kuti kavu Simiyu

1 July 2025, 5:12 pm

Kwenye picha ni kaimu meneja wa mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA kanda ya ziwa mashariki,Aggrey Muhabuki akizungumza na wamiliki wa maduka ya dawa muhimu mjini Bariadi Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Bado tunasafari kubwa sana katika kuelimisha jamii ya watoa huduma wa dawa  muhimu za binadamu maana wengi wao wanakiuka mashariti ya leseni zao bahati mbaya sana hata wanaohudumiwa nao wanaingia kwenye makosa yale yale”.

Na, Daniel Manyanga 

Mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA kanda ya ziwa mashariki amewataka wamiliki na wauzaji wa maduka ya dawa muhimu za binadamu kufuata sheria, kanuni , taratibu na miongozo ya uendeshaji wa maduka hayo Ili kujiepusha na mkono wa sheria kutokana na makosa ya ukiukwaji wa  leseni zao walizopewa na mamlaka husika.

Picha ya pamoja ikiwaonesha wamiliki wa maduka ya dawa muhimu wakifuatia jambo Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Hayo yamesemwa na kaimu meneja wa mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA kanda ya ziwa mashariki ,Aggrey Muhabuki wakati akizungumza na wauzaji pamoja na wamiliki wa maduka  katika halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu na kueleza kuwa maduka ya dawa muhimu yamekuwa yakitumika kinyume na mashariti ya leseni.

Muhabuki ameongeza kuwa Kuna maduka mengine wanalaza wagonjwa ambapo ni kinyume cha sheria kulingana na leseni walizopewa na mamlaka husika hivyo amewataka wamiliki wa maduka hayo kufuata miongozo wanayopewa.

Sauti ya kaimu meneja wa mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA Kanda ya ziwa mashariki

Aziza Hamis ni katibu wa afya wa mkoa wa Simiyu ambaye amevitaja vitendo vya ukiukwaji wa sheria vinavyofanywa katika maduka ya dawa muhimu mkoani Simiyu huku kaimu mfamasia wa mkoa wa Simiyu ,Philemon Mtinda akieleza kuwa hatua zinazochukuliwa kwa wauzaji wanaokiuka sheria zimesaidia kurekebisha mienendo yao.

Sauti ya katibu wa afya mkoani Simiyu na kaimu mfamasia mkoa wa Simiyu

Baadhi ya wamiliki wa maduka ya dawa muhimu mkoani Simiyu wameshaurielimu itolewe zaidi hususan maeneo ya vijijini ili kuwasaidia wananchi kuwa na uelewa juu ya huduma sahihi wanazopaswa kuzipata katika maduka ya dawa muhimu.

Sauti ya mmoja wa wamiliki wa maduka ya dawa muhimu,Dkt.Robert Mayongela