Sibuka FM

MEK wapigwa msasa kuwatambua wenye mahitaji maalum Bariadi

10 June 2025, 10:24 am

Kwenye picha ni wanafunzi wenye mahitaji maalum wakiwa kwenye picha ya pamoja Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Hakuna sheria inayobagua watoto kutokana na mapungufu ya kimaumbile, binadamu wote kwa Mungu wetu sote tupo na haki hivyo ni wakati sasa kwa jamii kuachana na imani kuwachukulia watoto wenye mahitaji maalum kama vile ni mkosi, tuwapatie mahitaji yao kama watoto wasiokuwa na ulemavu wowote wa kimwili”.

Na, Daniel Manyanga 

Wazazi na Walezi wenye watoto walio na mahitaji maalum wilayani Bariadi mkoani Simiyu wametakiwa kutowaficha ndani badala yake wawapeleke shuleni kwa ajili ya kupata haki yao msingi kwa mjibu wa sheria na haki za watoto bila kujali mapungufu waliyonayo.

Rai hiyo imetolewa na Afisa Elimu Maalum wa halmashauri ya wilaya ya Bariadi, Nasuna Henry wakati akizungumza na maafisa elimu, maafisa ustawi wa jamii na maendeleo ya jamii kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuwabaini na kuwatambua watoto wenye mahitaji maalum kwa ufadhili wa mradi wa shule bora huku mratibu wa mradi huo katika halmashauri ya wilaya ya Bariadi, Felister Mwanga, amesema kuwa mafunzo hayo kwa washiriki yatawasaidia kutambua watoto wenye mahitaji maalum kwa weledi zaidi kwa kushirikiana na walimu.

Sauti ya afisa elimu maalum na mratibu wa mradi wa shule bora

Kwa upande wao Enock Pwele na Rutherford Magayane ambao ni wawezashaji wa mafunzo hayo wameeleza namna ambavyo yatawasaidia washiriki wa mafunzo hayo kufanya kazi ya ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalum kwa weledi.

Sauti ya wawezeshaji wakielezea matumaini yao kwa washiriki katika kutambua na kubainisha watoto wenye mahitaji maalum

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo, Maro Msami ambaye ni afisa elimu kata ya Ngulyati na Wamdenge Kalingonji ambaye ni afisa ustawi wa jamii wa halmashauri ya wilaya  ya Bariadi wamesema kuwa mafunzo hayo  yatawawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi tofauti na hapo mwanzo kabla ya kupata ujuzi huo.

Sauti ya washiriki wa mafunzo wakielezea namna ambavyo mafunzo yatawasaidia kutambua watoto wenye mahitaji maalum ili waweze kupata haki ya elimu