Sibuka FM

TAKUKURU Simiyu yaokoa bilion 6 kwenye sekta ya elimu

28 May 2025, 7:51 pm

Kwenye picha ni mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) mkoa wa Simiyu, Manyama Tungaraza akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Kumaliza rushwa hapa nchini ni changamoto kubwa sana maana hata watumishi umma waliokula kiapo cha uaminifu ndiyo wanakuwa watu na viongozi wa kwanza katika kutekeleza ubadhilifu wa mali za umma halafu hao hao ndiyo wanahimiza uzalendo haya ni maajabu kweli”.

Na, Daniel Manyanga

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) mkoa wa Simiyu imeokoa  zaidi ya bilioni sita za miradi ya sekta ya  elimu iliyojengwa chini ya kiwango katika miradi inayotekelezwa mkoani hapo kutokana na fedha zilizoletwa na serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania katika kuboresha miundombinu ya elimu.

Kwenye picha ni muonekano wa nje wa jengo la taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) mkoa wa Simiyu Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Hayo yamesemwa na mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) mkoa wa Simiyu ,Manyama Tungaraza wakati akitoa taarifa ya kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/25 ofisini kwake mbele ya waandishi wa habari.

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Simiyu,Manyama Tungaraza akizungumza na waandishi wa habari katika kutoa taarifa za utekeleza wa robo ya tatu ya mwaka 2024/25

Manyama amesema kuwa mradi wa shule ya sekondari ya wavulana Simiyu ambapo baadhi ya miundombinu ya mradi kujengwa juu ya bomba la maji safi hatua iliyopelekea mradi huo kuchelewa kwa takribani siku 119.

Sauti ya mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Simiyu,Manyama Tungaraza akielezea namna ambavyo uchunguzi umefanikiwa kuepusha uhujumu wa mradi