Sibuka FM

Sangamwalugesha yaomba kujengewa soko la kisasa

27 May 2025, 11:19 am

Kwenye picha ni muonekano wa nje wa soko kuu la Maswa mjini ambapo ni moja wapo wa miradi iliyotekelezwa katika kuwawekea mazingira mazuri ya kufanya biashara hasa kwa wajasiliamali Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Uchumi wetu unajengwa na wajasiliamali wadogo wadogo hivyo tuna kila sababu kwa mamlaka husika kuwatengenezea mazingira mazuri ya wao kufanya biashara ikiwemo miundombinu ya masoko pamoja na kuangalia tozo ambazo hazina afya kwa wafanyabiashara”.

Na, Daniel Manyanga

Kukosekana kwa soko la uhakika la kufanyia biashara kwa wakazi wa mji mdogo wa Sangamwalugesha uliopo kata ya Sangamwalugesha wilayani Maswa mkoani Simiyu kumetajwa kuchangia kudorora kwa biashara maeneo hivyo wameomba kujengewa soko ili waweze kuuza, kununua bidhaa mbalimbali hali ambayo itakuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii nzima ya maeneo jirani.

Doto Salum ni mkazi wa kijiji hicho amewasilisha hoja hiyo mbele ya mkuu wa wilaya ya Maswa wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi ambapo ameuliza swali kwa nini mji huo mdogo hauna soko la uhakika licha ya kwamba eneo lipo la kujengewa miundombinu hiyo ili iwe rahisi kwa wafanyabiashara kufanya biashara zako kwa uhakika tofauti na hivi sasa wanauzia majumbani kwao.

Sauti ya mwananchi akitoa ombi kwa mkuu wa wilaya ya Maswa la kujengewa soko la kisasa wakati wa mkutano wa hadhara

Doto Salum na Dadas Maulid wamesema kuwa uwepo wa soko hilo kuwasaidia kununua ,kuuza na kufanyabiashara  hali itakayoondoa wafanyabiashara makanjanja wenye kuwaibia wakulima na wauzaji pamoja kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na jamii nzima ya maeneo jirani.

Sauti ya wananchi wakielezea namna ambavyo uwepo wa soko utasaidia kuinua uchumi wa wananchi wa eneo husika

Akijibu changamoto hiyo mkurugenzi mtendaji wa halmshauri hiyo, Maisha Mtipa akaahidi kulifanyia kazi swala hilo hivyo wananchi wawe na uvumilivu wakati serikali inatafuta namna bora ya kuwa soko maeneo hayo.

Sauti ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Maswa,Maisha Mtipa akizungumza na wananchi katika kujibu maombi ya kujenga kwa soko la kisasa