Sibuka FM

UVCCM Maswa kuwaunga mkono vijana uchaguzi mkuu

20 May 2025, 5:08 pm

Kwenye picha alivalia kofia ni mwenyekiti wa uvccm Maswa, Emmanuel Cosmas akiongoza moja wapo wa kikao akiwa na baadhi ya wajumbe wa umoja wa vijana wa uvccm Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

‘‘Vijana ni nguvu kazi ya taifa hili hatupaswi kabisa kuwa tunalalamika kulingana na viongozi wetu ambao tuliwaamini tukawapa kura za kuwa wawakilishi wetu kwenye vyombo vya maamuzi kwa sheria za nchi hii unaruhusiwa kugombea udiwani,ubunge kuanzia miaka 21 hivyo vijana hii ndiyo nafasi yetu pekee ya kufanya maamuzi ya kuwania nafasi za uongozi ili tuwe kwenye vyombo vya kutoa dira ya maendeleo uchaguzi huu tunatarajia kuwaona vijana wakiwania nafasi mbalimbali’’.

Na. Daniel Manyanga

Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) wilayani Maswa mkoani Simiyu wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika October .25 mwaka huu nchini ili wawe sehemu ya kutoa maamuzi na mustakabali wa taifa hili.

Akizungumza katika kikao cha baraza la UVCCM wilayani Maswa, katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Ephraim  Kolimba, amewataka vijana hao kuacha kuwa tegemezi na badala yake wajitokeze kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Sauti ya katibu wa CCM Maswa, Ephraim Kolimba akiwataka vijana wa CCM kuacha kuwa tegemezi badala yake wajitambue na kuwania nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu

Awali akizungumza katika kikao hicho, mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Maswa Emmanuel Cosmas, amesema kuwa umoja huo upo tayari kuwaunga mkono vijana wote watakaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Sauti ya mwenyekiti wa uvccm Maswa akielezea utayari wao kuwaunga mkono vijana katika uchaguzi mkuu ili waweze kushika nyadhifa mbalimbali
Kwenye picha ni mwenyekiti wa uvccm MaswaEmmanuel Cosmas akiwa kwenye moja ya shughuli za chama Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Kwa upande wao Lucia Christian,Emmanuel Samwel na Catherine Daniel  na vijana wa UVCCM wilayani Maswa wameeleza utayari wao wa kushiriki uchanguzi kwa  kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwa ngazi ya kata na majimbo  kwenye  uchaguzi mkuu mwaka huu.

Sauti ya vijana wakielezea utayari wao kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi mkuu
Matukio katika picha za pamoja wakati wa kikao na baada ya kikao cha umoja wa vijana wa uvccm Maswa Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm